FACEBOOK KUFUTWA????

Mark Zuckerberg, mwanzilishi na mwenyekiti wa mtandao wa Facebook ametangaza (kwa mujibu wa mtandao wa weekly world news) kwamba anaipiga chini Facebook ifikapo Machi 15.

"Facebook inanishinda nguvu", alisema Mark alipokutana na waandishi wa habari katika ofisi zake zilizopo Palo Alto, "Msongo wa kazi wa kuendesha wavuti hii umeharibu kabisa maisha yangu. Sasa ni wakati wa kumaliza kabisa wendawazimu huu."

Mark alikwenda mbali zaidi na kusema kwamba ifikapo Machi 15 hakuna mdau hata mmoja wa Facebook atakayeweza kutumia wavuti hili kubwa.
"Baada ya Machi 15, wavuti lote litakuwa marehemu," alisema Avrat Humarthi, ambaye ni makamu mwenyekiti wa sekta ya kiufundi katika Facebook. "Hii ina maana iwapo utataka kuendelea kuona picha zako basi hakikisha unaziondoa kwenye wavuti yetu na kuzihifadhi katika tarakilishi yako. Hutaweza kuziona tena mara Facebook itakapokula mweleka."
Mark alisema anaamini kabisa kwamba uamuzi wa kuifutilia mbali Facbook ni mgumu lakini hautawatibua wadau wa wavuti hili kubwa duniani.

"Kwa mtazamo wangu sidhani hata kidogo kwamba jambo hili ni la kumkoseha mtu usingizi", alisema katika mahojiano aliyofanya kwa njia ya simu. "Na kwa kiasi kikubwa nadhani hili ni jambo jema, kwa sababu sasa watu itawabidi kutoka kwenye maficho yao na kwenda kukutana na marafiki uso kwa uso, hili ni jambo jema."
Baadhi ya wadau wa Facebook walisikika wakiporomosha mitusi mara baada ya kusikia habari hizi.

"Huyu bwana anaongea upuuzi gani, anadhani mie ntaishije bila Facebook? Huu ni uzuzu!" alisema Denise Bradshaw, mwanafunzi wa sekondari huko Indiana. "Maisha yangu yote yamefinyangwa na Facebook, nimo kwenye wavuti hili karibu masaa kumi kwa siku. Sasa wewe unadhani ntakuwa nafanya nini katika masaa yote hayo?"

Lakini inasemekana kwamba wazazi wengi huko nchini Marekani wamezipokea habari hizi kwa shangwe, nderemo, vifijo, hoihoi, na mavuvuzela.
"Nashukuru Mungu kwamba ndoto mbaya ya Facebook inafikia mwisho," alisema Jon Guttari, ambaye ni mzazi huko Detroit. "Hatimae sasa nitapata wasaa wa kuwa karibu na mwanangu badala ya kuwa akipoteza muda wote kwenye tarakilishi yake. Nadhani sasa tunaweza kuwa na mazungumzo nyumbani."

Wanaofaidika kifedha na Facebook wamekuwa watu wa mwanzo kabisa kumpa kubwa Mark kwa kutupilia mbali dili hii ambayo inasemekana kuwa na thamani ya dola bilioni 7.9.
Lakini Mark amekuwa kichwa ngumu na amesema mpango wake wa kuachana na wavuti hili uko palepale."Sina mpango na hata senti moja inayotokana na wavuti hili kwa sasa, nataka maisha yangu ya awali."

Facebook Corporation imeshauri wadau wake wote kuondoa kila wanachokihitaji katika mtandao huu kabla ya Machi 15. Baada ya tarehe hilo kila kitu kitatoweka katika mtandao wa internet.
Ebwana Dah! na kama vipi hii inaweza ikawa ni publicity stunt, jamaa atakuwa kafanikiwa sana
Kutoka Kijijini kwetu www.Fotobaraza.ning.com

No comments: